Saturday, August 9, 2014

INDIA WAJITOA KWENYE KOMBE LA DUNIA NI BAADA YA KUZUIWA KUCHEZA MPIRA WAKIWA PEKU



  • Kombe la dunia mwaka huu ndio kombe la kwanza la dunia kutumia teknolojia ya goli ( goal-line technology) kwani haijawahi tokea kombe lolote la dunia ambalo limewahi kutumia teknolojia hii zaidi ya kutumia uwezo binafsi wa marefa na vibendera.

 

  • katika fainali zote mashindano ya kombe la duniani  zilizo wahi kuchezwa ni fainali mbili tuu ambazo ziliamuliwa kwa mikwaju ya penati fainali hizo ni za mwaka  1994 pale Brazil walipoifunga Italy na fainali nyingine ni ya mwaka 2006 pale Italy ilipoifunga France
 
  • Mpaka leo hii kombe la dunia linatimiza miaka 80 huku likizunguka katika nchi mbalimbali na mabara mbalimbali lakinkombe la kwanza la dunia lilifanyika katika nchi ya uruguay mwaka 1930 na nchi kumi na tatu (13) zilishiriki
    
  •  Vivian Richards raia wa antigua ndiye mwanamichezo pekee duniani kucheza na kushiriki  kombe la dunia akiwa na timu mbili za michezo tofauti alishiriki kombe la dunia kama mchezaji wa mpira wa miguu mwaka 1974 katika mechi za kufuzu, pia ni nguli nchini mwao katika mchezo wa cricket ambako pia ameshawahi kushiriki katika  kombe la dunia la cricket.
  •   Mashindano ya kombe la dunia ndiyo mashindano maarufu kuliko yote na yenye watazamaji wengi zaidi duniani kila mwaka yanapofanyika, mashindano hayo hutazamwa na watu zaidi ya bilioni nne duniani kote.

  • ·   licha ya Ujerumani kuifunga Brazil goli saba moja katika kombe la dunia mwaka 2014 lakini haishikirii rekodi ya kufunga magoli mengi katika kombe hilo , timu inayoshika rekodi kwa kufunga magoli mengi katika mechi moja ni Hungary ambayo iliifunga  El Salvador magoli   10 – 1  mwaka 1982.

  • ·  Haya kweli ni maajabu ya kombe la dunia usishangae watoto wa kibongo wakicheza chandimu wakiwa  peku nchi ya India ilijitoa katika mashindano ya kombe la dunia mwaka 1950 pale uongozi wa FIFA ulipowazuia kucheza peku katika mechi zao.




 

No comments:

Post a Comment